10 March 2016

WAACHENI WATOTO WADOGO WAJE KWANGU MAANA UFALME WA MUNGU NI WAO



TUWASAIDIE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUMU, NI WATOTO WETU NA WADOGO ZETU
Tunapozungumzia watoto wa mitaani kila mtu ana uelewa wake juu ya hilo na kwa muonekano anao uona yeye,

         MTOTO WA MTAANI:
Ni mtoto ambaye anayeishi katika mazingira ya kutangatanga  mitaani bila ya kuwa na sehemu maalumu ya kuishi na kutopata mahitaji muhimu anayotakiwa kupata mwanadamu,
Kama vile  chakula,maradhi na nguo.

           Tunapoangalia kwa muono wetu watoto wa mtaani wako wa aina tofauti tofauti na wamekuwa watoto wa mtaani kwa sababu tofauti tofauti.


Kila mtu ana historia yake katika maisha ama mbaya au nzuri ya enzi za utoto wake, wapo ambao wakikumbuka nyuma wanalia na kuichukia dunia maana walikosa tumaini na faraja toka utotoni mwao. 

Leo hii sisi tuliokwisha ona angalau mwanga katika hii dunia ni vyema tukawa tumaini au faraja nzuri kwa watoto wote wenye mahitaji maalumu katika jamii, tukiwasaidia kuanzia malezi bora, elimu bora lakini pia kunyanyua na kuvumbua vipaji vyao ili kuvikuza waje kuwa zao jema ukubwani, wasije wakalia na kuichukia dunia kama wengine, ni jukumu letu kama jamii, kujali, kuthamini na kutambua wajibu wetu kwa hawa watoto. 

Kuna makundi mbalimbali ya watoto ambao bila kujitoa kwetu kwa ajili yao ni sawa na kuandaa kizazi ambacho kwao furaha na upendo vitakuwa ni vitu vya kuvisikia kwa wengine, pia ni sawa na kuandaa kizazi chenye chuki na hasira na matokeo yake ni kujiingiza katika vitendo visivyo vya kiungwana.



MTOTO WA MTAANI ANAYETOKANA NA KUFIWA NA WAZAZI: 
Huyu ni mtoto ambaye aliyekuwa akilelewa malezi yote anayestahiki kupewa mtoto na katika mstari uliokuwa sahihi.



Mara nyingi watoto wa aina hii pindi wanapofiwa na wazazi huwa wanapitia tabu nyingi sana na kuwapelekea kuwa watoto wa mitaani, Pindi tu pale wanapofiwa na wazazi ndugu wenye tama za mali ujifanya wanapenda kukaa na watoto wa aina hii na kuwanyanyasa katika mali za wazazi wao na mwisho wake ni kuwafukuza katika majumba wanayoacha wazazi wao,

Inasikitisha sana kumuona mtu ni YATIMA alafu bado tena anaenda kuwa mtoto wa mtaani wakati wazazi wake wamemuachia kila kitu na wamewalea katika mstari ulonyoka,


ENYI WAZAZI/WALEZI: mnawachukua watoto wa ndugu zenu kwa kuwataka kuwalea kwa tama za mali tu na si kwa mapenzi ya dhati,sasa tubadilike na tuseme inatosha.

Kuondokewa kwa wazazi si mwanzo wa mtoto kuitwa mtoto wa mtaani na kupata mateso makubwa ambayo hayastahili, tuwapende  watoto wa ndugu zetu na tuwalee kwa moyo mkunjufu na wa upendo, hakika Mungu  atawalipa mema tu


MTOTO WA MTAANI ANAYETOKANA NA KUTELEKEZWA NA MZAZI/MLEZI: 

huyu ni mtoto wa mtaani anayesababishiwa na mzazi au mlezi mwenyewe kuitwa mtoto wa mtaani, Utakuta mzazi au mlezi amemzaa mtoto vizuri na akawa ana mlea lea lakini baadae akaona maisha magumu au ana taka arudi tena kwenye ujana kama mwanzo, mambo haya uwaga wanafanya sana WANAWAKE kama ulikuwa unaona maisha magumu  ulikubali vipi kuzaaa au unataka uwe kijana kila siku, mnaona mtelekeze watoto pahali popote pale na kuwakimbia kwa kuwadanganya utarudi kumbe ndo kwa kheri, kina mama tubadilike tuwe na mioyo ya uruma kwa watoto wetu na kuwapenda kwa hali yoyote ile,kama ulivyomuweka tumboni miezi tisa na ukamzaa kwa uchungu.


WANAUME: kina baba wengi upenda kutelekeza familia zao zikitanga tanga ovyo bila ya sababu za msingi mitaani, na kuwapelekea watoto kuitwa watoto wa mitaani kwa kukosa mahitaji muhimu sana sana maradhi mtoto hata njiani analala hana sehemu ya kuishi


Watoto hawa wanaotokana na kutelekezwa wanasikitisha sana katika jamii, wazazi na walezi wa pande mbili wanaume na wanawake, tujitahidi katika malezi ya watoto wetu, tusiwaache kwa kuwatelekeza wakawa watoto wa mitahani tunaopofanya maamuzi  yufikirie mara mbili mbili maamuzi yetu, wazazi wa pande mbili wote tushirikiane ili kupunguza ongezeko  la watoto wa mitaani, tumuogopeni MUNGU tutaenda jibu nini kesho kwake, wazazi tujitaidi kuwalea watoto wetu na tuache tabia ya kutelekeza watoto wasiokua na kosa.


WATOTO WA MITAANI WANAOTOKA MKOA MMOJA KWENDA MWINGINE:
Watoto wa mitaani hawa ni wale wanaochukuliwa mikoani kwa lkudanganywa wanakuja kusomeshwa na watu ambao wanawachukua, kumbe lengo kubwa la watu wengi wanaowagiza watoto kutoka mikoani au kuwafuata vijijini kwa kuwa labda wanatoka kijiji kimoja lengo lao kubwa ni kuja kuwafanyisha kazi watoto wa watu na kuwatesa  na kuwafukuza kama mbwa na kuwaacha wakitanga mitaani kwa kuwa awana ndugu wala jamaaa  mkoa walopelekwa,japo kuna wengine wanaokaa na watoto wa watu vizuri mungu awazidishie.

 
ENYI WAZAZI: mnaotoa watoto wenu ovyo kwa tamaaa labda ya vijihela mbadilike na muwapende watoto wenu msipende wakawa watoto wa mitaani na hali ya kuwa wazazi mpo hai, na kwa NYIE mnaowachukua watoto wa wenzenu na kuwaleta mikoa mingine kuweni na roho za huruma jamani na muwapende watoto wa wenzenu mtoto wa mwenzio ni mtoto wako pia,

JAMII KWA UJUMLA: Tumeona watoto wa MITAANI wanapatikana kwa njia tofauti tofauti, wewe kama mzazi au mlezi au mtanzania na una uzarendo na nchi yako tujitaidi kuwaangalia kwa jicho la umakini na la uruma watoto wetu wa MITAAN. na tuwe kipau mbele kuwasaidia na kuwatunza  katika jamiii yetu, tuachane na fikra na mawazo potofu na tuache tabia ya kuwatenga tukawaacha bila msaada.


SERIKALI: Ijitaidi kujenga mashule mengi ili kuepukana na watoto wa MITAANI  na kuweza kuongeza Vituo vya  kuwalea watoto hawa wa mtaani, pia ituwezeshe mashirika ua taasisi zinazosapoti jitihada hizi za kuwasaidia watoto hawa Yatima na watoto wa mitaani.

  Mtanzania kuwa mzarendo  na kuwa na huruma kwa WATOTO WETU WA MITAANI, tunakuhitaji wewe mtanzania Pamoja na Fahari Foundation tushirikiane kwa pamoja kupunguza ongezeko la watoto wetu yatima na watoto wa mtaani.

JAMII IWAJIBIKE KUWASAIDIA WATOTO WA MITAANI, YATIMA
Kitanda usichokilalia, huwezi kujua kunguni wake, shida na mateso wanayoyapata watoto waishio katika mazingira hatarishi na wale wa mitaani ni vigumu kueleza. Watoto hawa hawajui leo au kesho yao watakula nini, hakuna anayeangaika kuwatafutia chakula, wanapolala na njaa hakuna wa kumlilia, na wakiumwa hakuna wa kumweleza, hivyo huendelea na maisha yao hadi wanapopata nafuu au kupona kabisa.


Ukweli ni kwamba, watoto hawa hujisikia wapweke na wenye kudhoofika moyini kutokana na jamii kubwa kuwakataa na kuwaweka katika fungu tofauti. Jambo la kusikitisha, idadi kubwa ya watoto hawa ni kwamba umri wao unaanzia miaka miwili (2) hadi kumi (10), ambao kimsingi hawajui kujitegemea, njaa ikiuma wanalia tu bila tegemezi wala msaada na kushindwa kujieleza.

 Kitanda chao ni barabarani na wengine huona msaada wao ni kulala mitaroni, baridi yote ya usiku na jua la mchana ni lao, hawajui kubadilisha nguo zao, zile walizovaa wiki kadhaa zilizopita hadi leo hazijatoka mwilini mwao, Tumezowea kuwaona watoto wenye wazazi wakitoka nyumbani asubuhi na wazazi wao na kurudi majumbani mwao jioni wakiwa wamenawiri na wenye Amani na furaha. 

Watoto hawa yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi hawana pa kwenda, popote wanalala, chochote wanakula, hawana zuri wanalokutana nao, Jamii imesahau kuwa watoto hawa ni sawa na wao, wanasikia njaa kama watoto wao, baridi na maumivu sawa na wenzao, lakini nani anashughulika nao?


Fahari Foundation Imeliona hili na inakuomba wewe ushirikiane nasi ili kuwasaidia yatima hawa kuwarudishia furaha yao, Amani yao, kwa kuwatoka katika maumivu makubwa na mateso ya usiku na mchana, kuwapa mahali pa kulala, chakula, mavazi, matibabu na hata elimu.

Tukumbuke kua Watoto hawa hawakuchagua kuwa yatima na kuishi mitaani, na wala hawakuchagua kufiwa na wazazi wao na wala hawakupenda kutelekezwa na wazazi au walezi wao, wamejikuta wapo mitaani na hawana la kufanya kama watoto wetu wanavyojikuta wakiwa mikononi mwetu na wanapata kila kitu. Wahenga wanasema, kinga ni bora kuliko tiba. 

Fahari Foundation Kushirikiana na Mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO`s) na yale ya kimataifa na Serikali, kwa Pamoja tunasisitiza kushughulikia tatizo la watoto hawa wakiwa tayari mitaani. Jambo la msingi, nguvu inayotumika kuwasaidia watoto hawa ingepaswa kuelekezwa kwenye kinga ili kutibu tatizo hilo kabisa.



Sababu moja wapo inayochangia ongezeko la yatima na watoto wa mitaani ni migogoro isiyokwisha katika ndoa, Manyanyaso ya kijinsia, ubaguzi wa watoto, Pamoja na unyanyasaji wa kijinsia, mila n.k

Hatua za haraka zinahitajika ili kupunguza au kumaliza tatizo la watoto wa mitaani na yatima kwa kuwaunganisha na walezi pamoja na ndugu zao ambao tunaamini wapo.
Umefika wakati wa serikali kuratibu nguvu za mashirika haya na NGOs kwa kuhakikisha mashirika hayo, jamii na wao wenyewe wanachukua hatua stahiki kuhakikisha tatizo hilo nchini linakwisha...

Fahari Foundation inachukua mstari wa mbele kuwatetea watoto hawa walio katika hatari kubwa ya maisha yao wasipojua kesho yao, Kula kwao, kulala kwako kwa shida na taabu, kuugua kwao.


MIMI, WEWE NA YULE TUWE SEHEMU YA FURAHA KWA HAWA WATOTO.
Miaka takribani saba iliyopita kwenye mtaa fulani hapa Nchini katika usiku wa giza zito uliofunikwa na baridi kali iliyochangamana na ukungu, wapo vijana kadhaa wamelala chini ya mitaro, wamesogeleana karibu ili angalau wapate joto katika miili yao. Mashuka yao ni maboksi yaliyotolewa vitu vya thamani na kutupwa jalalani.


Kati ya vijana hawa ambao wamelala chini ya moja ya mitaro nilikuwepo mimi nimesimama pembeni yao ambapo kabla ya miaka saba iliyopita nilikuwa nikiishi nyumbani kwetu Ifakara, wilayani Kilombero mkoani Morogoro.

Huko nilikuwa nikiishi na wazazi wangu wote wawili, lakini baadaye wazazi wangu waliachana kufuatia kutokuwepo maelewano baina yao. Baba yangu akahamia Njombe na mama yangu akabakia Ifakara.

“Baada ya wazazi wangu kuachana maisha yalikuwa magumu pale nyumbani Ifakara hivyo mama akanishauri nimfuate baba hapa Njombe, nilifika Njombe na kuonana na baba yangu ambaye tayari alikuwa ameoa mke mwingine”, anasema Kijana huyo.
Maisha yangu na mama mpya hayakwenda vizuri kwani mama huyo hakunipenda. Chuki, kazi nyingi na kugombezwa zikanifanya baba mzazi kutafuta chumba maeneo ya Mgendera na kunipangishia mwanaye. Aliendelea kuhadithia kijana huyo.

Kama walivyo wazazi wengine wasiojali, baba yake akaanza kumtelekeza kijana wake taratibu na hatimaye mawasiliano kati yao yakafa kabisa. Shida nyingi zikamfika kijana huyo na moja ya shida hizo ni chakula na pango la nyumba.

“Nakumbuka baada ya baba kunitelekeza maisha yakabana zaidi, hapo ikabidi niwe naelekea mjini kutafuta kazi ambazo pia sikupata hali iliyopelekea kufukuzwa katika chumba alichokuwa amenipangia baba huku mwenye nyumba akaninyanganya kitanda ili kufidia kodi yake.” Aliendelea kusema kijana huyo.

Baada ya kuwa amefukuzwa katika chumba alichokuwa akiishi Kijana huyo aliamua kuingia mtaani, akawa mmoja wa watoto wa mtaani, huko maisha mapya ya ubabe, utumiaji madawa ya kulevya, Ulawiti, kesi za kusingiziwa wizi, kuomba kwa wapita njia, na kufukua jalalani akitafuta chakula na vyuma chakavu ikawa sehemu yake ya maisha.


“Maisha ya mtaani yalikuwa machungu zaidi ya kifo unachokijua. kila siku mimi na watoto wengine walionikaribisha mtaani tulizurura kila kona tukitafuta chakula, mavazi na malazi… nilijawa hofu sana, sikuwa na raha Zaidi ya wasiwasi mwingi ulizunguka maisha yangu.. lakini ningefanya nini!? Hapana, sikuwa na namna ya kufanya… nilijipa moyo nikajikaza kiume na kuendelea na maisha”.

Nilichojifunza kikubwa ni kwamba mitazamo hasi ya jamii kuhusu watoto wa mitaani mara nyingi imekuwa chachu ya kufanya maisha ya watoto hawa kuwa magumu na hivyo kuwalazimisha kufanya matukio mengine ambayo katika maisha yao hawakuwahi kufikiria kuyafanya.


Kijana huyu anabainisha wazi kwamba ipo sehemu ya jamii inawaona watoto wa mtaani kama nuksi, vibaka, wabakaji. Na kwa sababu hiyo wameamua kuwapa mgongo. 

“Kwa kuwa jamii na serikali imetutenga hii inakuwa fursa ya wakora wengine kututendea watoto wa mitaani matendo maovu wayatakayo, siku moja tukiwa tumelala katika moja ya mitaa ya Njombe tulivamiwa na kundi la watu wanaotuzidi umri wanaonekana kuwa na maisha safi, wakawashika watoto watatu kati yetu mimi na baadhi ya wenzangu tukakimbia, ajabu wale watu waliwalawiti wale watoto wenzangu, zingatia kuwa umri wa watoto wenzangu ulikuwa kati ya miaka 10 mpaka 13.”

 “katika kipindi nilichokuwa nikiishi mtaani wapo wachache waliotusaidia sisi watoto wa mtaani, lakini kibaya zaidi wale ambao mnawaita matajiri, wenye pesa zao na magari ya kifahari hapa Njombe na wanaoishi kwenye nyumba zilizondani ya kuta za gharama kubwa hakuna hata mmoja kati ya hao aliyewahi kutusaidia” aliongeza.

Badala yake kijana huyo aliueleza kuwa msaada mkubwa waliupata kutoka kwa masikini na watu wenye kipato cha kawaida. 

Nilipomuuliza kuhusu wapi alipo baba yake, hivi ndivyo alivyosema kijana huyo,
“Baada ya kukaa muda mrefu bila ya kuonana ama kuwasiliana na baba yangu baadaye nilipata taarifa kuwa alifariki dunia siku nyingi, natamani ningeweza kumuona japo kwa mara ya mwisho ama kufahamu wapi kaburi lake lilipo niende kulitembelea lakini haijawa hivyo, kwa hili nasikitika sana.”


Kijana huyo kwa sasa anaishi katika kituo cha kulea watoto waishio katika mazingira magumu cha ‘Compasion’ cha Airport mjini Njombe, anakiri na kushukuru kufika hapo kwani kituo kinamsomesha kwa gharama zake. Hivi sasa yupo kidato cha pili katika shule ya sekondari ya Mpechi. 

Kijana huyu ni mjuzi pia wa masuala ya umeme pamoja na utengenezaji madishi ya Luninga, kupitia kipawa alichonacho unaweza kumpa ajira ambayo mwisho wa siku ikampatia kipato na hivyo kumpa maisha bora.

"Haya maisha mpaka lini"?
Ni maneno ya huyu mtoto ambaye hajui atakula nini na atalala wapi?

JAMII YA KITANZANIA TUNA KILA SABABU YA KUWASAIDIA HAWA WATOTO

 

No comments:

Post a Comment